Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Monday, September 28, 2015

picha za mafuriko ya Lowassa tanga yaliyosababisha mkutano kuahirishwa

Read More »

Saturday, September 26, 2015

CCM Yarusha Jeshi La Anga Kuwakabili UKAWA Likiongozwa Na Mwigulu Nchemba.......Hapa Kuna Picha Wakipiga Push-Up Kumpa Sapoti Magufuli



Makada imara wa CCM  Field Marshall Mwigulu Nchemba na Dkt. Hamis Kigwangalla waki-Magufulika kuonesha sapoti kwa Mgombea wao Dkt. John Pombe Magufuli aliyefanya tukio hilo siku si nyingi kwenye Jukwaa la Kampeni.
Field Marshall Mwigulu Nchemba akilakiwa kwa nderemo mjini Nzega

Dkt Hamisi Kigwangalla akiwasili kwenye Ufunguzi wa kampeni za Ubunge jimbo la Nzega Mjini.Mjumbe wa timu ya Ushindi ya Chama cha Mapinduzi Field Marshall Mwigulu NChemba ambaye  ameanza safari za Anga-kwa-Anga kusaka kura Nchi nzima,Hapa akizungumza na Wananchi wa Nzega namna CCM ilivyosimamisha Mgombea Bora wa Urais ambaye sifa yake kuwa ni KAZI TU na rafiki yake Mkubwa ni TANZANIA. Comrade  Mwigulu amesema, Uchaguzi wa mwaka 2015 ni mwepesi sana kwa CCM  kwa kuwa wagombea wote ni zao la Chama tawala  na wanawajua vizuri. 
 Mbunge Ubunge wa jimbo la Nzega Mjini Ndg. Hussein Bashe akizungumza na Wananchi wake wakati wa Ufunguzi wa kampeni kwa Jimbo la Nzega Mjini. Bashe amewaomba Wana-Nzega kumpatia ridhaa ya kuwa mbunge wa Jimbo hilo ili aweze kusimamia vyema shughuli za Maendeleo kama Uimarishaji wa Huduma za Afya kwa Hospitali ya Nzega, Kusimamia haki za Bodaboda na Mamantilie wa Nzega, shughuli za Halmashauri ya Mji wa Nzega kwa Ufanisi.Pia amesisitiza yeye ni TEAM MAGUFULI na anaamini Maendeleo ya kweli na ya kasi yataletwa na Magufuli kwa awamu hii ya tano ya Uongozi wa Taifa letu.Mbunge Mtarajiwa wa Chama cha Mapinduzi Jimbo jipya la Nzega Vijijini Dkt. Hamis Kigwangala akisalimiana na Wananchi wa Nzega mjini alipokwenda kusapoti Ufunguzi wa kampeni za Mgombea Jirani Ndg.Hussein Bashe. Picha zote na Sanga Festo Jr

Read More »

Friday, September 25, 2015

Huu ndio Mfano wa KARATASI YA KURA YA WAGOMBEA URAIS 2015

Read More »

Top 10 Richest Premier League Owners 2015

Manchester City is the 2nd richest Premier League club 
Mansour bin Zayed Al Nahyan
Read More »

Wednesday, September 23, 2015

CHEKI PICHA HATARI ZA SHAMSA FORD

Read More »

Tuesday, September 22, 2015

hizi ndio smartwatchez za kununua kwasasa


Read More »

Emmanuel Mbasha Aachiwa Huru...Upande wa Mashtaka Umeshindwa Kuthibitisha kosa la Ubakaji dhidi yake

Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini, Emmanual Mbasha (32), leo ameangua kilio baada ya kuachiwa huru na Mahakama ya Wilaya ya Ilala huku mke wake, Flora amesema yuko tayari warudiane endapo ataomba radhi.

Mbasha alimwaga chozi muda mfupi baada ya kutoka katika chumba cha Mahakama alipopandishwa kizimbani kusomewa hukumu.

Mshtakiwa huyo ameachiwa huru dhidi ya kesi ya ubakaji iliyokuwa ikimkabili baada ya upande wa mashtaka kushindwa kudhibitisha kosa.

Mwimbaji huo ambaye kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo alionekana hana furaha, alifikia uamuzi huo wa kulia mara tu baada ya kusomwa kwa hukumu hiyo, ambapo alipotoka nje ya chumba cha mahakama alipiga magoti chini huku akiinua mikono juu na kulia kwa sauti huku akisema ‘mungu ni mwema’.

Mbasha anakabiliwa na mashtaka mawili ya kumbaka shemeji yake mwenye umri wa miaka 17 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria

Kesi hiyo namba 186 ya mwaka 2014, imeendeshwa kwa mwaka mmoja na miezi miwili na kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Juni 17 mwaka 2014.

Akisoma hukumu hiyo leo, hakimu Mkazi Flora Mujaya alisema mahakama imemuachia huru baada ya upande wa mashtaka kushindwa kudhibitisha kosa lililokuwa likimkabili.

“Mahakama yangu imemuachia huru Mbasha baada ya upande wa mashtaka kushindwa kudhibitisha kosa ”alisema Hakimu Mujaya.

Hakimu Mujaya alisema mahakama hiyo imetoa uamuzi huo baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi sita wa upande wa mashtaka vikiwemo vielelezo vilivyotolewa mahakamani hapo kama ushahidi.

Hukumu hiyo, ilipaswa kutolewa wiki iliyopita , lakini iliahirishwa hadi leo kwa sababu hakimu huyo ambaye ametoa hukumu hiyo leo alikuwa likizo .

Mke wa Mbasha, Flora alisema yeye na familia yake wanaheshimu maamuzi yaliyotolewa na Mahakama dhidi ya Mbasha na kwamba anaiomba familia yake ikubaliane na maamuzi hayo na suala la kukata rufaa lisiwepo.

“Mimi na familia yangu tunaheshimu uamuzi wa mahakama na ninaiomba familia yangu ikubaliane na uamuzi huu uliotolewa na mahakama na suala la kukata rufaa lisiwepo kwani uamuzi wa mwisho upo katika familia” alisema Frola alipotafutwa kwa simu.
Read More »

Wednesday, September 16, 2015

Diamond Platnumz apokea ushindi wa tuzo nyingine mbili

dai2
Headlines za Diamond Platnumz haziishii hapo, good news kwako mtu wangu msanii wetu wa Bongo Flava anazidi kuonyesha ubora wake kwenye nafasi mbalimbali za tuzo Africa… Diamond amepokea ushindi wa tuzo nyingine tena! African NAFCA Awards 2015 imemtaja Diamond kuwa Msanii wa mwaka anaependwa na wimbo wa ‘Nana’ umetajwa kuwa Wimbo wa mwaka unaopendwa!
Read More »

Picha 5 kutoka ndani ya Studio ya Clouds FM wakati DJ Fetty anatangaza kuacha kazi ya utangazaji…

Jina lake ni Fatma Hassan aka DJ Fetty, moja ya Watangazaji ambao wamepata majina makubwa sana TZ na East Africa kutokana na kazi ya Utangazaji ambapo ana mchango mkubwa pia kwenye muziki wa Bongo Fleva kama Mtangazaji wa show ya Entertainment, XXL ya Clouds FM.
 
 September 15 2015 Show ya XXL inaandika Historia nyingine tofauti ambapo DJ Fetty ametangaza kuacha kazi ya Utangazaji na kuingiza nguvu yake zaidi kwenye masuala ya Biashara… wakati Fetty anatangaza hivyo, presenter mwingine pia Kened the Remedy ameungana na Timu ya XXL kwa mara ya kwanza

 

Ndani ya Studio ya Clouds FM, hapo yuko Kennedd, Adam Mchomvu, DJ Zero, B Dozen na DJ Fetty.
Read More »

Tuesday, September 15, 2015

Adebayor aondoka Tottenham


Mshambuliaji wa kilabu ya Tottenham Emmanuel Adebayor ameondoka katika kilabu hiyo baada ya makubaliano ya pande zote mbili.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kutoka Togo alikuwa hajaichezea Spurs msimu huu na alikuwa amewachwa katika vikosi vya kucheza ligi ya Uingereza pamoja na ile ya Yuropa.
''Tunamuombea mema katika maisha yake ya baadaye',ilisema taarifa ya Tottenham.
Adebayor aliyewasili katika kilabu ya Manchester City kwa kitita cha pauni milioni 5 mwaka 2012,alikuwa amesalia na mwaka moja katika kandarasi yake na alikuwa akitaka kulipwa pauni milioni 5 ili kusitisha kandarasi hiyo mapema.
Hatahivyo kilabu ya Tottenham haijatangaza makubaliano ya usitishwaji wa kandarasi hiyo.
Akizungumza mapema juma hili ,kocha mkuu wa Tottenham Mauricio Pochettino alisema kuwa Adebayor hakuwa katika 'fikra zake' ama hata mpango wa mbeleni wa timu ya Tottenham.
Read More »

PICHA YA LOWASSA INAYOZUA UTATA MTANDAONI

Read More »

Lori Lavamia Msafara wa Magufuli

MSAFARA wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, umenusurika kupata ajali, baada ya lori la mizigo kuuvamia na kugonga magari matatu likiwamo lililokuwa limembeba mpiga debe wa chama hicho, Amon Mpanju.

Ajali hiyo ilitokea jana asubuhi katika eneo la Njia Panda jirani  kilomita chache kabla ya kuingia Maswa mjini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Gemin Mushi jana alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Alisema wakati msafara huo ukitoka wilayani Meatu, askari polisi waliokuwa wakiuongoza msafara huo walimuaru dereva wa lori hilo lenye namba za usajili T 217 DDY kuegesha pembeni gari lake, lakini alikaidi.

“Msafara wa mgombea urais ulikuwa jirani kuingia Maswa, dereva wa lori aliamuriwa kuliweka pembeni akakaidi, tena kibaya akaongeza mwendo hali iliyosababisha ajali.

“Lori hili ni mali ya Kampuni ya Dilchadri Mill Ltd ya jijini Mwanza, liligonga magari matatu likiwamo gari lenye namba za usajili T 217 CYM aina ya Toyota Land Cruser ambayo iliharibika vibaya na kushindwa kuendelea na safari.

“…Baada ya tukio hili, dereva amekimbia na polisi wanamsaka ili  afikishwe mbele ya vyombo vya sheria,” alisema Kamanda Mushi.

Kutokana na ajali hiyo, Kamanda  Mushi amewataka madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani.Alisema hakuna mtu aliyeumia katika ajali hiyo.

Wakati huo huo, mgombea huyo aliendelea na mikutano yake katika wilaya za Maswa, Kishapu na Igunga.

Kwa nyakati tofauti katika mikutano hiyo, Dk. John Magufuli, aliwataka Watanzania kuchagua wabunge ambao watatetea masilahi yao badala ya wale wanaotoka bungeni kila zinapowasilishwa bajeti.

Alisema endapo atachaguliwa anataka kuona Bunge linalotimiza wajibu wake, ikiwemo kupigania  kero za waliowachagua.

“Haiwezekani wakati wa kujadili hoja za wananchi, wenzako wanatoka nje wanafanya hivi kwa kumkomoa nani?

“Maswa ninyi ni mashahidi kwa muda mrefu hamkuwa na mtu wa kuwasemea tatizo la maji, barabara na hata huduma za afya. Maana kila zinapopangwa bajeti wao wanatoka nje je waziri atajuaje kama kuna tatizo eneo husika.

“Hii si demokrasia hata kidogo ila ni kuwatesa wananchi, kwa hali hiyo sasa Watanzania wote chagueni wabunge wenye masilahi kwenu na watakaosemea shida zenu na si wale wanaotoka nje kila wakati (Ukawa),” alisema Dk. Magufuli

Aonya lugha chafu
Alisema ni vema viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kampeni za matusi, kwani hazina tija kwa Taifa.

“Matusi si hoja, ndiyo maana kila ninaposimama situkani mtu, najenga hoja. Tunahitaji kujenga nchi yetu iwe ya amani siku zote,” alisema.
Read More »

Friday, September 11, 2015

Kanisa Katoliki Sasa Kuvunja Ndoa

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis jana alieleza mabadiliko mapya yanayolenga kuwarahisishia Wakatoliki kuvunja ndoa zao na kuoa upya.

Dhamira hiyo ni ishara nyingine ya dhamira ya Papa huyo kutaka kulifanya Kanisa Katoliki liwe rafiki zaidi na kuendana matakwa ya walio wengi.

Akizungumza kuhusu mabadiliko hayo, Papa alisema si haki kwa wenzi kuishi muda mrefu ‘wakikandamizwa na wingu la shaka’ kuhusu uhalali wa ndoa zao.

Ikumbukwe kwamba ni msimamo wa Papa kumkatalia Mfalme Henry the VIII wa Uingereza kumtaliki mkewe Catherine wa Aragon katika karne ya 16 uliosababisha England ijitenge na Rome na kushuhudia kuundwa kwa Kanisa la England huku mfalme akiwa mlinzi wa Imani wa kanisa hilo.

Mabadiliko makuu matatu aliyotangaza  Papa jana ni   kuondoa mchakato wa mapitio ya mara ya pili wa uamuzi wa kutoa talaka kupitia mahakama ya kanisa kabla ya ndoa kuvunjwa.

Mengine ni kuwapatia maaskofu uwezo wa kuharakisha na kuvunja ndoa   wenzi wanapoamua wenyewe katika mazingira fulani kama vile ukatili katika ndoa au uasherati na mchakato huo wa talaka kuwa bure, isipokuwa kwa kulipa ada ndogo kwa ajili ya gharama za  utawala.

Kabla ya sheria hiyo, Wakatoliki waliotaka talaka walihitaji kibali kutoka kwa mahakama mbili za kanisa, wakati sheria mpya inabakiza moja ingawa rufaa bado zinaruhusiwa.

Kabla ya sheria hiyo, wanandoa wa Wakatoliki wanaotalikiana bila idhini ya kanisa na kuolewa upya walihesabiwa kama wazinifu na hawakuruhusiwa kupokea komunio.

Lakini kwa mujibu wa  utaratibu mpya, wanaotalikiana wakioa au kuolewa tena watabakia kuwa wafuasi wa kanisa hilo.

Mwaka jana Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa hilo  kuboresha na kurekebisha taratibu hizo  kurahisisha wanandoa kuachana na kupunguza gharama.

Mageuzi hayo yalikuja katika mfumo wa nyaraka mbili zinazoitwa ‘motu proprio’, neno la kilatini lililobuniwa na Papa mwenyewe.

Taratibu hizo zitakuwa rasmi kama sehemu ya sheria za kanisa (canon law) ifikapo Desemba 8 mwaka huu wakati Papa atakapoanza kutangaza Mwaka wa Jubilee ambao kwa kawaida huhusishwa na msamaha.
 
Read More »

Tuesday, September 8, 2015

LOWASSA ALETA UDINI KWENYE KAMPENI ZAKE ASEMA NI ZAMU YA WALUTHERI KUONGOZA, MAGAZETI SEPREMBER 8



















Read More »