Bunge la Ugiriki limeidhinisha kura
ya maoni iliyokuwa imetishwa na waziri mkuu wa nchi hiyo Alexis Tsipras
kuhusu mpango wa kuisaidia kiuchumi nchi hiyo uliopendekezwa na
wakopeshaji wake.
Akizungumza kabla ya kura hiyo, bwana Tsipras
amewataka watu nchini Ugiriki kupiga kura ya hapana kwenye kura ambayo
itafanyika tarehe 5 mwezi Julai.Amewalamu wakopeshaji wa nchi hiyo wakiwemo muungano wa ulaya, benki kuu ya Ulaya na shirika la fedha duniani kwa kuihangaisha ugiriki.
Amesema kuwa kura ya hapana itaipa ugiriki uwezo wa kufanya majadiliano.
No comments:
Post a Comment