Gereza hilo la Guantanamo, ambalo limepewa jina la umaarufu kuwa Gitmo - limekuwa likitumiwa na Marekani kuwazuilia wapiganaji kutoka vita vya Iraq na vya Afghanistan bila kufunguliwa mashtaka yoyote. Rais Obama alitoa agizo la kirais kufungwa kwa kituo hicho mara moja katika siku yake ya kwanza. Lakini baraza la Congress lilikataa kuwahamisha wafungwa wa huko kuwaleta nchini Marekani kutokana na hofu za kiusalama.
Wengi tayari wamerejeshwa nchini mwao japo kunao baadhi ambao wanaaminiwa kuwa hatari zaidi na hivyo hawaja achiliwa.
Msemaji mmoja wa ikulu ya white house ameambia waandishi kuwa mipango ya kuwasafirisha wafungwa hao kwa njia salama imefikia awamu za mwisho na itawasilishwa kwa baraza la Congress, lakini hakutoa maelezo zaidi.
No comments:
Post a Comment